Top-ads

By | 8:08 AM

Taswira Mbalimbali Za Muendelezo Wa Operesheni Okoa Kusini inayofanywa na CHADEMA


 Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akihutubia maelfu ya wananchi Masasi mjini
Mbunge wa jimbo la Ubungo (CHADEMA) John Mnyika akipandisha bendera ya chama nje ya ofisi ya CHADEMA Kijiji cha Mkangaula
  Pichani ni Mwenyekiti Freeman Mbowe akikata utepe wa kufungua Ofisi ya CHADEMA Kijiji cha Mkangaula. Ilikuwa ni baada ya Katibu Mkuu, Dkt. Slaa kutoa hotuba ya ufunguzi na John Mnyika kupandisha bendera ya chama nje ya ofisi hiyo, ikiwa ni ishara ya kupiga hatua katika mapambano ya awamu ya pili.
 Mbunge wa Ubungo(CHADEMA)John Mnyika akitoa 'somo' kwa wanakijiji wa vijiji vya Kata ya Lumesule. Mapema Mbunge wa Ubungo(CHADEMA)John Mnyika alikaribishwa na kuzungumza na Katibu wa Tawi wa CUF, Bi. Zaituni. Wananchi walimwelewa vyema.



 John Mnyika akiwa katika vijiji vya Kata za Makukwe na Mkwedu, wilayani Newala. Kwa George Mkuchika ambako alikutana na kiashiria cha wazi kuhusu udhaifu wa Waziri Mkuchika (Mbunge wa Newala) katika kusimamia majukumu yake, baada ya wananchi katika Kijiji cha Tengulengu, Kata ya Mkwedu kumlalamikia kuwa Diwani wa Kata hiyo, Juma Dadi hajawahi kufungua ofisi yake zaidi ya mwaka mmoja sasa. Pamoja na kuwasilisha malalamiko yao kwa barua Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Newala na kwa Mbunge wao, Mkuchika, hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.
 Unaweza kuona pia wanawake wakiitikia PEOPLES POWER, nao wakaipiga ya nguvu kweli kweli kuonesha umoja na mshikamano katika Falsafa ya Nguvu ya Umma ya CHADEMA, katika kudai uwajibikaji, kupigania haki, uhuru na mabadiliko ya kweli ya mfumo na utawala nchini.
 
 Sehemu ya Umati mkubwa wa wananchi kwenye mkutano huo
Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Slaa akizongwa na wananchi wa Kijiji cha Namahinga, Masasi aliokuwa akisalimiana nao.
 Opresheni Okoa Kusini katika picha, hapa ilikuwa Masasi Mjini. Waweza kuona katika baadhi ya picha watu walivyopanga mstari kupigania kadi.Picha na Habari na Kurugenzi ya Habari- CHADEMA

Tawi la CHADEMA Washington DC Nchini Marekani Lazidi Kuvuna Wanachama Wapya



  Linda Bezuidenhout (LB) furaha baada ya kuvua kamba kuvaa kwanda na kuchukua kadi  kuwa mwanachama kamili wa Chama Cha Demokrasia Chadema.
 Mwenyeketi wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe. Kalley Pandukizi, pamoja na katibu wake  Mhe. Libe Mwang'ombe akimkabidhi rasmi mwanacham mkareketwa  ambae ni mwana mitindo Linda  Bezuidenhout (LB) kati ya uwanachama wa chama cha  Demokrasia Chadema katika ofisi ya  tawi la Tawi la Chama Washington DC.
 Mwenyeketi wa  Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Kalley Pandukizi akiwa na katibu wachama hicho,Ndugu Libe Mwang'ombe alipotoa kadi rasmi kwa Beautician maharufu na designer wa kitanzan Linda  Bezuidenhout (LB)
 Viongozi wa tawi la chadema Washington DC wakipata Champagne
Mwenyeketi wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe.  Kalley pamoja na katibu wake  Mhe. Libe Mwang'ombe wakipata picha ya pamoja na Linda  Bezuidenhout Atlanta, Georgia na wanachama wa tawi la chadema Washington DC. Katika miaka ya nyuma Linda aliwahi  kusponsor  matukio mbali mbali kwenye  miaka ya 1990 wengi wao wakimjua kwa Linda Express Nchini Tanzania ambae ambaye hivisasa anajishughulisha na  biashara ya nguo za kiume milanovita.com pamoja na  zakike ambazo anadesign mwenyewe kwa brand name ya Linda kutoka Atlanta, Georgia Nchini Marekani.Picha na Mdau Wa Swahilivilla
Newer Post Older Post Home