Taswira Mbalimbali Za Muendelezo Wa Operesheni Okoa Kusini inayofanywa na CHADEMA
Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akihutubia maelfu ya wananchi Masasi mjini
Mbunge wa jimbo la Ubungo (CHADEMA) John Mnyika akipandisha bendera ya chama nje ya ofisi ya CHADEMA Kijiji cha Mkangaula
Pichani
ni Mwenyekiti Freeman Mbowe akikata utepe wa kufungua Ofisi ya CHADEMA
Kijiji cha Mkangaula. Ilikuwa ni baada ya Katibu Mkuu, Dkt. Slaa kutoa
hotuba ya ufunguzi na John Mnyika kupandisha bendera ya chama nje ya
ofisi hiyo, ikiwa ni ishara ya kupiga hatua katika mapambano ya awamu ya
pili.
Mbunge wa Ubungo(CHADEMA)John Mnyika akitoa 'somo' kwa wanakijiji wa vijiji vya Kata ya Lumesule. Mapema
Mbunge wa Ubungo(CHADEMA)John Mnyika alikaribishwa na kuzungumza na
Katibu wa Tawi wa CUF, Bi. Zaituni. Wananchi walimwelewa vyema.
John
Mnyika akiwa katika vijiji vya Kata za Makukwe na Mkwedu, wilayani
Newala. Kwa George Mkuchika ambako alikutana na kiashiria cha wazi
kuhusu udhaifu wa Waziri Mkuchika (Mbunge wa Newala) katika kusimamia
majukumu yake, baada ya wananchi katika Kijiji cha Tengulengu, Kata ya
Mkwedu kumlalamikia kuwa Diwani wa Kata hiyo, Juma Dadi hajawahi
kufungua ofisi yake zaidi ya mwaka mmoja sasa. Pamoja na kuwasilisha
malalamiko yao kwa barua Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Newala na
kwa Mbunge wao, Mkuchika, hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.
Unaweza
kuona pia wanawake wakiitikia PEOPLES POWER, nao wakaipiga ya nguvu
kweli kweli kuonesha umoja na mshikamano katika Falsafa ya Nguvu ya
Umma ya CHADEMA, katika kudai uwajibikaji, kupigania haki, uhuru na
mabadiliko ya kweli ya mfumo na utawala nchini.
Sehemu ya Umati mkubwa wa wananchi kwenye mkutano huo
Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Slaa akizongwa na wananchi wa Kijiji cha Namahinga, Masasi aliokuwa akisalimiana nao.
Opresheni
Okoa Kusini katika picha, hapa ilikuwa Masasi Mjini. Waweza kuona
katika baadhi ya picha watu walivyopanga mstari kupigania kadi.Picha na Habari na Kurugenzi ya Habari- CHADEMA
Tawi la CHADEMA Washington DC Nchini Marekani Lazidi Kuvuna Wanachama Wapya
Linda Bezuidenhout (LB) furaha baada ya kuvua kamba kuvaa kwanda na kuchukua kadi kuwa mwanachama kamili wa Chama Cha Demokrasia Chadema.
Mwenyeketi
wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe.
Kalley Pandukizi, pamoja na katibu wake Mhe. Libe Mwang'ombe
akimkabidhi rasmi mwanacham mkareketwa ambae ni mwana
mitindo Linda Bezuidenhout (LB) kati ya uwanachama wa chama
cha Demokrasia Chadema katika ofisi ya tawi la Tawi la
Chama Washington DC.
Mwenyeketi
wa Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Kalley
Pandukizi akiwa na katibu wachama hicho,Ndugu Libe Mwang'ombe alipotoa
kadi rasmi kwa Beautician maharufu na designer wa kitanzan
Linda Bezuidenhout (LB)
Viongozi wa tawi la chadema Washington DC wakipata Champagne
Mwenyeketi
wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe.
Kalley pamoja na katibu wake Mhe. Libe Mwang'ombe wakipata picha ya
pamoja na Linda Bezuidenhout Atlanta, Georgia na wanachama wa tawi la
chadema Washington DC. Katika
miaka ya nyuma Linda aliwahi kusponsor matukio mbali mbali kwenye
miaka ya 1990 wengi wao wakimjua kwa Linda Express Nchini Tanzania
ambae ambaye hivisasa anajishughulisha na biashara ya nguo za kiume milanovita.com pamoja na zakike ambazo anadesign mwenyewe kwa brand name ya Linda kutoka Atlanta, Georgia Nchini Marekani.Picha na Mdau Wa Swahilivilla