Top-ads

SIKUWAHI PIGA PICHA ZA UCHI ILI NIWE MAARUFU....SHILOLE

By | 8:50 AM
MSANII ndani ya tasnia ya filamu na muziki, Zena Muhamed ‘Shilole’, ameamua kuongea kuwa awali alipoigia kwenye tasnia ya filamu alikuwa anatafuta skendo lakini hata hivyo hakuwahi kujiweka nusu uchi ili ajulikane kwani siku ambayo atafanya hivyo ananaamini hata familia yake na hata mashabiki wanaomkubali watamuona mtu wa ajabu sana"nilikuwa natafuta skendo kipindi cha nyuma lakini si kwa kukaa uchi" aliongea msanii huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri mnoo na kundi lake lenye staili ya kanga moko.
Msanii huyo alidai kuwa alikuwa na skendo nyingi lakini hakuwahi kuwaonesha watanzania mwili wake kama baadhi ya wasanii wanavyofanya, kwani kitendo hicho endapo angeamua kukifanya basi wazazi wake wangemchukulia kama limbukemi wa maisha ya mjini.


Kauli ya msanii huyo inakuja ili kujisafisha kwani wadau wengi wa tasnia ya filamu kwa sasa hawana hamu nayo, kutokana na vitendo vingi vinavyofanywa na wasanii wake, ambapo vingine vimekuwa vikiwahawaribu hata watoto wadogo ambao hupenda sana kutazama kazi zao.
Newer Post Older Post Home